Published September 2, 2019 | Version v1

UKOPAJI WA LUGHA: ETIMOLOJIA NA MABADILIKO YA MAANA NA UTAMKAJI WA MSAMIATI WA KIARABU KATIKA KISWAHILI.

Authors/Creators

  • 1. Chuo Kikuu cha Kenyatta

Description

Pindi wazungumzaji wa lugha mbili wanapotagusana na kuingiliana basi moja kwa moja lugha hizo huweza kukopana na kuathiriana kifonolojia, kimsamiati na kisarufi. Waarabu walipofika pwani ya Afrika Mashariki, walikumbana na Waswahili na hapo ndipo Kiswahili kikakopa maneno na sauti za kiarabu ambazo hazikuwepo katika lugha ya Kiswahili. Pili, Kiswahili pia kikachukua baadhi ya sauti za kiarabu na kuzibadili jinsi zinavyotamkwa. Makala haya yanatafiti na kuainisha etimolojia ya baadhi ya maneno ya kiarabu yanayopatikana katika lugha ya Kiswahili na jinsi sauti za kiarabu zilivyokopwa na kubadilishwa na kuswahilishwa.na pili namna baadhi ya maneno yalivyobadilishwa maana asilia baada ya kukopwa kutoka lugha ya Kiarabu. Nadharia za mfumo na semantiki tambuzi za msamiati zilitumika.

Files

14.pdf

Files (454.4 kB)

Name Size Download all
md5:bdf993c0030147d7c3ae61cd309281c5
454.4 kB Preview Download